Tuesday, September 13, 2011

WASHIRIKI WA MAFUNZO YA HABARI ZINAZOHUSU UNYANYAPAA WAPEWA VYETI

Afisa Habari wa PACT TANZANIA, Bi. Leah Mwainyakule akiwa na mwezeshaji wa mafunzo bw.Wilbroad Manyama

Mdau Abdulaziz Ahmed kushoto, wa Channel Ten akipokea cheti cha kufuzu mafunzo ya unyanyapaa kwa watoto na watu wanaoishi na VVU, anayekabidhi ni bw. Wilbroad Manyama akishuhudiwa na bi. Leah Mwainyakule

Baadhi ya Waandishi waliopata mafunzo hayo
Mdau Abdulaziz wa pili kutoka kushoto akiwa na Mdau Frank kutoka Iringa (kushoto) na wakati wa mafunzo

Waandishi wa habari kutoka mikoa Tisa ya Lindi, Mtwara, Iringa, Rukwa, Mbeya, Tanga, Dodoma, Morogoro na Dar Es Salaam wamepatiwa mafunzo ya siku tano ya unyanyapaa kwa watoto na watu wanaoishi na VVU.
Mafunzo hayo yaliyofanyika mkoani morogoro yameandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la PACT TANZANIA kwa lengo la kuwawezesha waandishi wa habari nchini kufahamu namna ya kuandika habari za unyanyapaa wa watoto na watu waishio na VVU.
 
Sambamba na mafunzo hayo ya siku tano waandishi hao pia walipatiwa nyeti vya kufuzu mafunzo hayo.
HABARI NA: Mdau Abdulaziz- Lindi.

No comments:

Post a Comment