Thursday, September 22, 2011

AFROKIJA YAZUNGUMZA NA KIDA WAZIRI


Naamini utakuwa unamkumbuka Mwanamama Kida Waziri (pichani) ambaye alitamba na Bendi ya Vijana Jazz na kujijengea heshima kubwa sana hasa kwa wanawake kutokana na vibao vyake vikali ambavyo vilibeba ujumbe mzito na wenye mafundisho, kama vile kibao Mawifi ambacho kimebeba ujumbe wa wanawake kuwanyanyasa wifi zao, kibao Penzi haligawanyiki ambacho kinazungumzia suala zima la mapenzi kama jina la wimbo linavyojieleza na vingine vingi tu.

Kida Waziri ambae kwa sasa amebadili dini na kutoka Uislam na kwenda Ukristo na kuokoka kabisaa ana Historia kubwa sana katika Muziki ambapo mpaka kufikia alipo sasa amepitia mambo mengi na kujifunza vitu vingi sana, mwenyewe anasema alikuwa akipenda Muziki tangu akiwa mdogo ila alikuwa muoga wa kupanda Stejini na kuimba mbele za watu na mara yake ya kwanza kufanya hivyo ilikuwa nchini Kenya ambapo alipata mshituko mkubwa sana na kushindwa kuendelea kuimba kutokana na watu kumshangilia sana kwa sauti yake na uimbaji wake kwa ujumla maana ndo ilikuwa mara yake ya kwanza kuimba na aliongopewa kuwa akiimba hatosikika hivyo yeye aliamini kuwa anaimba kwa kujifurahisha tu lakini si kwa kutoa burudani.

Na baada ya hapo akapewa moyo kuwa anaweza na ndo akapata moyo wa kuwa anaweza na kuamua Rasmi kuianza kazi hiyo ya Muziki, lakini aliporejea hapa Nchini Tanzania kutokea Kenya alipata mtihani mkubwa sana baada ya dada yake aliyekuwa akiishi nae kumzuia kuimba maana alikuwa akiishi jirani na na Mzee King Kikii hivyo akawa anamkaribisha mazoezini kwao ili aweze kuimba ila dada yake ndo hivyo akawa anamuwekea ngumu mpaka ikafikia wakatia akamfuata King Kikii na kumwambia kuwa akiendelea kufuatilia mdogo wake atamshtaki kwa wazazi wake kuwa anamfundisha tabia Mbaya Kida kwa kuwa alikuwa natumia muda mwingi mazoezini na hashiriki katika kazi za nyumbani, ila mwisho wa siku aliruhusiwa na ndo akaanza kuimba katika Bendi ya Jeshi hapa hapa jijini Dar Es Salaam na hatimaye akaangukia katika bendi ya Vijana Jazz na baadae akaachana kabisa na muziki mpaka mwaka huu alipoamua kurejea tena na kuamua kuzirekodi upya baadhi ya nyimbo zake za zamani na kutoa Album yake binafsi.

Ana Historia ndefu sana na yenye kuvutia ila hapa nimekupa kwa ufupi tu yale ambayo naamini wengi walikuwa hawayafahamu lakini kwa undani zaidi fuatilia Afrobeat ya Eatv ili upate kumsikia Livee!!!

No comments:

Post a Comment