Thursday, September 22, 2011

STEVE RNB AZIBA PENGO LA BOB RUDALA "INAFRIKA BAND"

Mwanamuziki ambaye anafanya vizuri kwenye gemu ya muziki wa Bongo Flava (Kulia)Steve Rnb ambae ametamba na vibao kadhaa kama vile One Love na Sogea karibu hatimaye ametua INAFRIKA Band ili kuziba pengo la Bob Rudala ambae ameihama bendi hiyo na kutimkia Kalunde Band. Akizungumza na blog hii Steve amesema ameamua kujiunga na bendi hiyo kwa kuwa ni bendi ya muda mrefu inayofanya vizuri hivyo anaamini atajifunza mengi sana kutoka kwa wanamuziki wa bendi hiyo, kwa kuwa sasa anafanya vitu vingi kama vile utumiaji wa vyombo mbalimbali tofauti na ilivyokuwa mwanzoni ambapo alikuwa akiimba tu.
Mmoja kati ya watunzi na waimbaji wa Bendi hiyo "Hamis" (pichani) amesema yeye binafsi anafurahia kufanya kazi na Steve kwa kuwa ni kijana anayejituma na ndio maana ameweza kuziba pengo la Bob Rudala, hivyo anatumai baada ya muda atakuwa mwanamuziki bora zaidi ya sasa kwa kuwa ameanza kupiga vyombo mbalimbali na anaendelea kujifunza kupiga vyombo vingine.
Akizungumzia kuhusu bendi kiongozi wa Bendi hiyo "Roy" amesema kwa sasa bendi yao imejipanga vizuri kulingana na soko la muziki kwa sasa na wanatarajia kutoa Album yao mpya itakayoitwa jina la Mbeleko wakati wowote kuanzia sasa hivyo mashabiki wakae tayari kuipokea Album hiyo.
Ukipenda kuiona kazi ya Steve Live fuatilia Afrobeat kila Jumamosi saa moja jioni, ili uone Steve Rnb anavyokung'uta Drums.

No comments:

Post a Comment