Tuesday, September 20, 2011

PRINCE AMIGO ATOA SOMO KWA WANAMUZIKI WENYE TABIA YA KUHAMA HAMA BENDI ZAO

Mwimbaji mahiri wa kundi la Taarab la Jahazi Modern Taarab Prince Amigo amekanusha uvumi uliokuwa umeenea mitaani kuwa ana mpango wa kulihama kundi lake hilo la sasa na kuhamia kundi jipya la Tanzania Moto.

Akizungumza na Blog hii Prince Amigo amesema ni kweli alifuatwa na uongozi wa kundi hilo(Tanzania Motto) ili aweze kujiunga nao lakini yeye binafsi alikataa kwa kuwa hakuwa na sababu ya kuihama Jahazi na kujiunga na kundi hilo. "Ni kweli kundi hilo lilinifuata lakini mimi binafsi sikuona sababu ya kuhama Jahazi na kujiunga na kundi hilo"

Amigo aliongeza kuwa yeye kama msanii anayejitambua hawezi kuhamahama bila kuwa na mipango kwa sababu kuhama bendi kila siku kunamfanya msanii adharaulike na kuonekana hana msimamo na hajui anachokifanya. "Unajua mimi kama msanii ambae najitambua na kuelewa nini ninachofanya siwezi kuhamahama ovyo kwani ukiangalia wengi ambao wana tabia hiyo hawana mafanikio na wanapotea kimuziki lakini wale wanaotulia tunaona mafanikio yao, mfano dada yangu Luiza Mbutu yeye ana mafanikio makubwa kwa sababu ametulia sehemu moja na anajitambua yeye ni nani hivyo mimi naiga mfano wake.

Mengi zaidi usikose kuangalia Afrobeat ya EATV jumamosi hii saa moja usiku.

No comments:

Post a Comment