Tuesday, September 13, 2011

NAUNGANA NA WATANZANIA WENZANGU KUTOA SALAMU ZA POLE NA RAMBIRAMBI KWA WENZETU WALIOATHIRIKA NA AJALI YA MELI

MV Spice ikiwa inazama

Baadhi ya ndugu wakijaribu kutambua miili ya ndugu zao katika picha

Kwa kweli aliyepakia magodoro amekuwa msaada mkubwa sana kwa kuwa baadhi ya watu waliokosa life jackets waliyatumia magodoro hayo ili kujiokoa

Vyombo vya usalama na wasamaria wema wakisaidia zoezi la uokoaji
Naamini kila mmoja wetu atakuwa ameguswa na maafa makubwa yaliyotokea usiku wa kuamkia Tar 10, Septemba ya kuzama kwa meli ya MV Spice na kusababisha mamia ya ndugu zetu kupoteza maisha na wengine kujeruhiwa, kama ambavyo tumeona na kusikia mengi yakizungumzwa na kufanyika hivyo basi nami kama mtanzania na binadamu ambae pia kwa namna moja au nyingine naguswa na matatizo mbalimbali yanayowakabili binadamu wenzangu napenda kutoa pole kwa wale wote ambao kwa namna yoyote ile wameguswa au kuathiriwa na maafa haya.

Huu si muda wa kuzungumza mengi sana ila la msingi ni kuwaombea ndugu zetu waliopoteza maisha walale mahali pema peponi na wale walionusurika kwenye ajali hiyo wapate nafuu mapema ili waweze kurejea katika shughuli zao za kila siku... AMEEN.

No comments:

Post a Comment