Wednesday, September 7, 2011

KIDA WAZIRI MBIONI KUTOA ALBUM YAKE

Kida Waziri katika pozi

Mwanamuziki wa enzi hizo wa bendi ya Vijana Jazz Kida Waziri (pichani) amejipanga kutoa Album yake binafsi ambayo itakuwa na nyimbo sita, ambapo nne kati ya hizo ni zile alizowahi kuziimba miaka ya 90 wakati akiwa na bendi yake hiyo.
Akizungumza jijini Dar Es Salaam Kida ambae ni mwanamke wa kwanza kuimbia Bendi ya Vijana Jazz amesema mpaka sasa anafikiria "wimbo wifi zangu" ndio utakaobeba jina la Album hiyo ambayo alianza kurekodi jijini Arusha kabla ya kuhamishia kazi hiyo jijini DSM ambapo anamalizia nyimbo zake zilizobaki.

Pamoja na wifi zangu Kida amesema nyimbo zingine za zamani zitakazokuwa kwenye Album hiyo ni Penzi haligawanyiki, Mary maria na Penzi haligawanyiki sehemu ya pili ambazo zote alishiriki kuziimba.
Amefafanua kuwa ameamua kurudia nyimbo hizo kwa kuwa anaamini watu wengi wangependa kuzisikiliza nyimbo hizo zikiwa zimerekodiwa kiustadi na sauti ya Kida kama ilivyokuwa ikisikika miaka ya nyuma.

Kida ameongeza kuwa kazi hiyo ya kurekodi ilikwishakamilika lakini baada ya kusikiliza alibaini baadhi ya mapungufu hivyo kulazimika kuzirudia baadhi ya nyimbo katika Studio za Dar Es Salaam.

No comments:

Post a Comment