Wednesday, September 14, 2011

KAMATI MISS TANZANIA YAWAOMBA RADHI WATANZANIA

Kamati ya mashindano ya urembo ya Miss Tanzania imewaomba Radhi watanzania na wale wote waliopatwa na maafa ya ajali ya kuzama kwa meli ya MV SPICE ISLANDER huko visiwani zanzibar, kwa kuendelea na shindano wakati Taifa likiwa kwenye majonzi mazito ya kuwapoteza watu zaidi ya 200.

Mratibu wa Shindano hilo Hashim Lundenga amesema kuwa kamati yake ililazimika kuendelea na Shindano hilo kutokana na kumalizika kwa muda wa kuwasilisha jina la mshindi kwenye shindano la Mrembo wa Dunia.

Lundenga aliongeza kuwa kamati yake ilipata taarifa hizo za Jumamosi saa 9:30 alasiri ambapo muda mfupi tu ulikuwa umebaki kabla ya shindano hilo kuanza, hata hivyo shindano hilo lilifanyika wakiwa latika maombolezo ambapo kabla ya kuanza shindano watu wote waliokuwepo ukumbini walisimama kimya kwa muda wa dakika moja kwa ajili ya kuomba na hata washiriki walipopita jukwaani kwa mara ya kwanza walikuwa wamevaa vitambaa vyeusi kuashiria maombolezo.

No comments:

Post a Comment