Wednesday, September 7, 2011

MARIAM BSS AKIRI KURUDISHA PESA TANZANIA MOTO

Mariam katika Interview na Afrobeat
Mariam na Mutoto muzuri "Kijah"
Mshindi wa BSS 2010 Mariam Mohamed, amefunguka kuhusu uvumi kuwa alikuwa na mpango wa kulihama kundi lake la sasa la Five Stars Modern Taarab na kuhamia kundi jipya la Tanzania Moto ambalo limeanzishwa hivi karibuni.

Akizungumza na kipindi cha Afrobeat kinachorushwa na Eatv, Mariam amekiri kuwa ni kweli alipata ushawishi wa kujiunga na kundi hilo kutokana na ushawishi wa pesa na ahadi nyingi ambazo alizipata kutoka kwa viongozi wa kundi hilo. "Unajua pesa ni shetani sana na shetani wa pesa ndiye alinishawishi kutaka kulihama kundi langu lakini baada ya kukaa na viongozi wangu wa Five stars na mimi mwenyewe kutafakari nilibadilisha uamuzi na kuamua kurudisha pesa ambazo walinipatia viongozi wa Tanzania moto" alisema Mariam.

Mariam ameongeza kuwa viongozi wa Kundi hilo walimpatia pesa taslimu Shilingi laki nne na nusu (450,000) za kulipia nyumba ili aweze kuhama nyumba anaishi sasa.. Hata hivyo amedai kuwa hata baada ya kurudisha pesa hizo viongozi wa Tanzania Moto bado wanaendelea kumshawishi kuhamia kundi hilo ambapo amekiri kuwa hatoweza kuhamia kundia hilo na hayuko tayari kuafanya kazi na kundi l;olote kwa sasa zaidi ya Five Stars kwani anaamini kuwa yeye ni muhimu na anahitajika sana kwenye kundi hilo.  

Usikose kuangalia Afrobeat Jumamosi hii saa moja jioni kwa hayo na mengine mengi ambayo Mariam ameyazungumza.

No comments:

Post a Comment