Friday, June 28, 2013

Rama Dee na Lady JD, hatimaye!

Wanamuziki wakongwe toka nchi Tanzania, Lady Jay dee na Rama Dee wamejipanga kutoa wimbo wa pamoja hivi karibuni, wakali hawa wanaaminika kuwa wanaweza sana miondoko ya R&B kwahiyo huo moto wake nahisi utakuwa balaa.

Rama Dee ambaye kimakazi anaishi nchini Australia kwa sasa amesema wimbo hoo ni kwaajili ya mashabiki wake pamoja na mwanadada Lady Jay Dee hivyo amesema anaomba sapoti yao maana bila mashabiki anaamini kuwa msanii hawezi fika kokote.

"Wimbo tumefanya mimi la Lady Jay dee na utatoka muda si mrefu, mashabiki wakae mkao wa kula maana tumejitahidi kadiri ya uwezo wetu ili kuhakikisha tunatoa wimbo ambao utawafurahisha mashabiki wetu na kuongeza ukaribu zaidi kwetu na wao".

Basi sawa, wananchi wanasubiri kwa hamu maana wengi walikuwa wana hamu ya kuona wawili hawa wakifanya kolabo, naamini maombi ya wengi sasa yamesikilizwa.

No comments:

Post a Comment