Friday, June 21, 2013

MHESHIMIWA MACHALI AMELAZWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA DODOMA BAADA YA KUVAMIWA NA MUPIGWA JANA JIONI

Mbunge wa Kasulu mjini Mh. Moses Machali amelazwa katika Hospitali ya Rufaa mjini Dodoma kufuatia kuvamiwa na kujeruhiwa na watu wasiojulikana katika maeneo ya Ipagala mkoani Dodoma.

Tukio hilo lilitokea jana jioni wakati Mh. Machalli akiwa kwenye gari lake baada ya kuwapigia honi vijana kadhaa waliokuwa katikati ya barabara ili wasogee pembeni ili naye aweze kupita .

  Vijana hao walioonekana kuchukizwa na kitendo hicho cha kupigiwa honi hivyo walianza kuishambulia gari hiyo ya Mh. Machali kwa kuigonga kwa nguvu jambo ambalo lilimfanya Machalli kusimamisha gari na kushuka ili kuzungumza na vijana hao waweze kufikia muafaka.

Baada ya Machali kushuka,  vijana hao walianza kumshambulia kwa matusi ya nguoni na ndipo Machalli aliamua kuwajibu kwa hasira kitendo kilichasababisha vijana hao waanze kumsahambulia kwa kumpiga.

Kwa mujibu wa shuhuda wa tukio hilo ni kwamba vijana hao waliompiga Mh. Machali walikuwa zaidi ya nane na ndiyo sababu ya yeye kushindwa kumsaidia Mheshimiwa huyo kwa kuhofia kuunganishwa katika kipigo.

Chanzo makini cha Blog hii kimemtembelea Mh. Machali Hospitalini hapo na kwamba wakati yeye akiwasili katiak Wodi namba 18 alimkuta akiwa amelala hivyo hakuweza kuzungumza nae chochote na kuzungumza na muuguzi wa zamu aliyefahamika kwa jina la Zainab na kusema kuwa walimpokea Mh. Machali majira ya saa 5 usiku jana ambapo alifikishwa na askari Polisi ambao walifika katika eneo la Ipagala alipovamiwa Mheshimiwa ili kumpa msaada na kufanikiwa kumkimbiza hospitalini hapo.

Aidha awali Mheshimiwa Machali mwenyewe alikiri kuwa anaamini kuwa watu hao waliomfanyia kitendo hicho ni wahuni tu kwa kuwa hana ugomvi na mtu yeyote kwa sasa hivyo hafikirii kama ni njama za watu fulani ila ni wahuni tu.

Hata hivyo taarifa zaidi zinasema kuwa eneo hilo la Ipagala si salama sana kwa sasa kwa sababu kuna vibaka wengi ambao hufanya matukio kama hayo ya uhalifu mara kwa mara.

Blog hii inamtakia kheri Mheshimiwa Machali aweze kupona ili arejee katika shughuli zake za ujenzi wa Taifa.




No comments:

Post a Comment