Thursday, June 27, 2013

Kaseja, Sunzu kwaheri Simba.


Uongozi wa Simba kuamua kumtema mchezaji wao Juma Kaseja wamesema imetokana na maneno ya watu yanayoendelea huko mitaani, hali inayosababisha wao kuamua kumuacha Juma Kaseja aende akajaribu sehemu nyingine.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, mwenyekiti wa Simba kamati ya usajili , Zakaria Hanspope alikuwa na haya ya kusema

“Unajua Juma Kaseja amechezea timu ya Simba kwa miaka mingi sana, laikini hivi karibuni kumezuka maneno ya ajabu kuhusu Juma Kaseja kuuza mechi anapokuwa uwanjani, kwahiyo kama uongozi tumeoa hali hii haitoleta picha nzuri kwa timu yetu.

Kiongozi huyo alidai kuwa sababu zingine hawatopenda kuziweka wazi ila kubwa ni kuhusiana Juma Kaseja kutoaminiwa na baadhi ya mashabiki na kudai kuwa , kwa sasa anapocheza uwanjani na timu zingine basi huwa anaamua kuuza mechi na kufungwa ili wapinzani waweze kushinda.

“Kwahiyo kama viongozi wa simba tumeona hali hii ya mashabiki kumsema kuwa Juma Kaseja anauza mechi kwa wapinzani, itapunguza kiwango chake cha uchezaji, hata yeye anaposikia haya maneno ile munkari ya kucheza inaisha kabisa sababu watu ambao anacheza kwaajili yao hawamuamini tena” Alisema Zakaria Hanspope

Aidha Zakaria Hanspope akielezea kuhusiana na mchezaji Felix Sunzu alisema kuwa masuala ya malipo ndiyo yameleta utata kati yao

“Felix Sunzu anataka tumlipe pesa kubwa zaidi ambayo ni dola 3500, ukingalia bajeti yetu kwa sasa hicho kiwango cha pesa ni kikubwa na itakuwa kazi kumlipa , kwahiyo tumeakuwa tukibishana katika malipo, yeye amesimamia kiwango hicho na sisi hatuna uwezo wa kumlipa hicho kiwango kwa sasa”. Alisema mwenyekiti wa Simba kamatii ya usajili, Zakaria Hanspope

No comments:

Post a Comment