Thursday, June 27, 2013

MWENYEKITI WA CHADEMA JOHN HECHE ASEMA NI AIBU KWA NCHI KUFANYA USAFI KWA SABABU YA WAGENI

Mwenyekiti wa Baraza la vijana Chadema (BAVICHA) John Heche (pichani)amesema, kitendo cha Serikali kuamuru usafi ufanyike katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar Es Salaam pamoja na kuwahamisha wafanyabiashara wanaofanya shughuli zao kandokando ya barabara kwa sababu ya ujio wa Rais wa Marekani ni aibu kwa Taifa.

Akizungumza leo jioni kwenye kipindi cha Hot Mix kinachoruka kupitia EATV, Heche alisema pamoja na sababu zinazodaiwa na viongozi wa serikali kuhusu kuhamishwa kwa wafanyabiashara hao, lakini moja ya sababu kubwa ni ujio wa Rais Obama anayetarajia kufika Nchini Julai 1 kwa ziara ya kikazi ya siku tatu na kusisistiza kuwa ni aibu kubwa kwa Taifa kwa maana hatuwezi kufanya usafi mpaka tusikie kuna wageni.

Akijibu swali la Mtangazaji wa kipindi hicho Adrian Hilary Stepp kuwa kwa nini vurugu hizo zinazotokea mara kwa mara wakati wa mikutano ya chama chao(CHADEMA) pekee na si vyama vingine vya upinzani, Heche alisema kwa sababu chama chao ndicho chenye nguvu na kinaipa Presha chama Tawala hivyo hufanya mipango hiyo ya vurugu ili kuwatisha wananchi wasihudhurie mikutano yao akitolea mfano wa vurugu za Arusha zilizosababishwa na kurushwa kwa bomu na kuongeza kuwa bomu hilo lilikuwa na mkono wa serikali.

No comments:

Post a Comment