Wednesday, June 26, 2013

TENDWA ATATANISHA WANANCHI


Msajili wa Vyama vya Siasa nchini John Tendwa,  amedai kuwa ikibainika kuwa CHADEMA ndio waliohusika katika kulipua bomu katika mkutano wao wa 15/06/2013 atakifuta.
Tendwa  ameyasema   hayo alipokuwa akizungumza katika kipindi cha Hot Mix cha East Africa Television akijibu swali la mtangazaji wa kipindi Adrian Stepp  kuhusu  hatua  zitakazochukuliwa...
Alipoulizwa kama itathibitika kuwa CCM ndio walihusika kulipua bomu hilo amedai kuwa hawezi kukifuta kwakuwa kwa kufanya hivyo itakuwa ni kufanya mapinduzi ya kalamu na jeshi linaweza kutawala nchi.
Pia  jaji Tendwa akiwa kwenye mjadala, amekanusha kuwa mhe Mizengo Pinda hakusema askari wapige wananchi, ni upotoshaji tu wa wanahabari na kuongeza kuwa wanahabari wanapaswa kumtafuta mhusika pale anapotoa habari ili kupata ufafanuzi zaidi wa habari hiyo.

No comments:

Post a Comment