Monday, June 17, 2013

MWILI WA MSANII LANGA KUAGWA NA KUZIKWA LEO KATIKA MAKABURI YA KINONDONI

Mwili wa aliyekuwa msanii wa muziki wa Bongo Fleva Langa Kileo(Langa) aliyefariki Alhamis ya wiki iliyopita, unatarajiwa kuagwa na kutolewa heshima za mwisho leo majira ya mchana nyumbani kwao Mikocheni jijini Dar Es Salaam na safari ya kuelekea katika makaburi ya kinondoni ambapo ndipo mwili wake utahifadhiwa itaanza majira ya saa 8 mchana.
Tunatoa pole kwa ndugu, jamaa, marafiki na mashabiki wa mwanamuziki huo na Mwenyezimungu aiweke roho ya marehemu Langa mahali pema peponi, Amina.

No comments:

Post a Comment