Monday, June 17, 2013

STEPS ENTERTAINMENT YATOA TUZO KWA WASANII WALIOFANYA NAO KAZI KWA MWAKA 2012/13

Baadhi ya wasanii wa kiume wa Bongo movie wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa tuzo zao za mwaka 2012 zilizoandaliwa na Steps Entertainment na kudhaminiwa na kampuni ya steps Solar
Mkurugenzi wa Kampuni ya Steps Entertainment bwana Dilesh Solanki akifafanua jambo kabla ya kumkabidhi tuzo ya mwogozaji bora wa filamu nchini kwa mwaka 2012 tuzo iliyochukuliwa na Mkurugenzi wa RJ Company bwana Vincent Kigosi(Ray) wakati wa utoaji wa tuzo hizo zilizofanyika usiku wa June 15 katika ukumbi wa Blue Pearl Hotel Ubungo jijini DSM na kuhudhuliwa na wasanii na wadau wa Filamu nchini.
Ridhiwani Kikwete (wa tatu kushoto) akiwapongeza baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya Kanumba the great iliyokuwa inamilikiwa na marehemu Steven Kanumba baada ya kuwakabidhi Tuzo ya Movie iliyofanya vizuri sokoni 2012/2013
Ridhiwani Kikwete (kushoto) akimkabidhi tuzo msanii Haji Adamu(Baba Haji) kwa niaba ya Jimmy Mponda aliyeshinda tuzo ya msanii bora wa Filamu za Action wakati wa utoaji wa tuzo hizo.
Riyama Ally akipokea Tuzo yake
Jacob Steven alichukua tuzo ya msanii bora wa kiume 2012/2013 wakati kwa upande wa wanawake tuzo hiyo ilinyakuliwa na mrembo Irene Uwoya
Mtoto Jenipher nae akipokea tuzo yake, ambapo aliliza wengi baada ya kushindwa kutoa neno la shukrani na alipofika sehemu ya kumshukuru Uncle JJ(Marehemu Kanumba) alishindwa kuendelea na kuanza kulia.
Msanii Nice Mohamed a.k.a Mtunisi akipokea tuzo yake ya filamu yenye ujumbe
Amri Athumani a.k.a Mzee Majuto nae akipokea Tuzo yake ya msanii bora wa vichekesho

No comments:

Post a Comment