Wednesday, June 26, 2013

KAMA MIPAKANI WANAFANYA UKAGUZI, MADAWA YA KULEVYA YANATOKA WAPI?



Leo ni siku ya kupambana na madawa ya kulevya kitaifa, na takwimu zinaonesha kuwa mkoa wa Dar Es Salaam unaongoza kwa kuwa na watumiaji pia waathirika wengi wa madawa ya kulevya, hii inatokana na mkoa huu kuwa na starehe karibia zote.
Mkoa  wa pili kwa biashara za madawa ya kulevya nchini Tanzania, unatajwa kuwa ni mkoa wa Tanga na hii inatokana na bandari ya Tanga, hivyo kusababisha shughuli za uingizaji wa madawa kutoka nje kufanyika katika eneo hilo kwa wingi, hali inayofanya wakazi wengi wa Tanga kupata madawa hayo kwa urahisi zaidi.
Madawa ya kulevya yanatajwa kuwa chanzo kikuu cha kuharibu akili ya mtu kwa kushindwa kujielewa na kufanya maamuzi yasiyo sahihi, hali hi husababisha mtu kushindwa kufanya kazi kwa usahihi na hali ya umaskini kumvaa kwa wingi.
Madawa ya kulevya yanasababisha tumkumbuke shujaa marehemu Amina Chifupa, aliyejitolea kupambana na madawa ya kulevya enzi za uhai wake ila harakati hizo zilisizi baada ya mh. Huyu kufariki dunia, hadi sasa bado hajatokea  mwenye harakati kama zake za kupambana na madawa ya kulevya.
Wanamuziki wengi wa hapa nchini Tanzania wamekumbwa na tatizo hili, tunakumbuka hata enzi za uhai wake mwanamuziki Langa Kileo aliwahi kukiri kutumia madawa ya kulevya na alisema kuwa ameacha kutumia madawa hayo baada ya kuona yanamharibia maisha yake.
Hii pia inatukumbusha kuwa vijana wengi kwa sasa madawa yanawaharibu sana, wapo wachache ambao ni watu maarufu tu ndio tunajua kuwa wanatumia, lakini kwa upande wa pili wapo watu wengi nchini Tanzania ambao sio maarufu na wanatumia haya madawa na wengi wao yanawaua na kusababisha taifa kupata hasara kubwa kila siku.
WITO KWA SERIKALI:
Katika hali ya kushangaza nchini Tanzania eti wanasema mipakani kuna watu wa kukagua madawa ya kulevya na kasoro zingine, uwanja wa ndege na hata bandarini kuna askari kibao wa kitengo cha madawa ya kulevya, swali linakuja.


 Je, huwa wanapokagua hao watu hawayaoni hayo madawa ya kulevya maana watu wanapita na hakuna anayekamwatwa lakini mwisho wa siku madawa unakuta yamesambaa kwa wingi nchini.
Imefikia wakati sasa serikali iache kucheza na akili za watanzania, mtu akiwa na madawa akamatwe na aadhibiwe masuala ya baadhi ya polisi kupokea rushwa na kuruhusu watu wa madawa ya kulevya kuyaingiza, yamepitwa na wakati, tunahitaji mabadiliko toka serikalini ili kufikia malengo ya millennia.

SAY NO TO DRUGS

No comments:

Post a Comment