Wednesday, January 16, 2013

ZAIDI YA ABIRIA 100 WANUSURIKA KUFA BAADA YA KIVUKO KUZIMA INJINI BAHARINI


ZAIDI ya watu 100 wamenusurika kufa maji baada ya Kivuko cha MV Magogoni kuzima injini na kupoteza mwelekeo baharini ambapo habari zinasema kuwa Kivuko hicho kilizima baada ya kupishana na meli kubwa ya Azam iliyokuwa imebeba mizigo na hata nahodha wa meli hiyo ya mizigo alifanya kazi kubwa ya kukikwepa kivuko hicho.


Akizungumza na blog hii jana, mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo Halima Fred ambaye ni mkazi wa Kigamboni aliyekuwa ndani ya kivuko hicho alisema, baada ya injini za Mv Mgogoni kuzima, nahodha alishindwa kuizuia isisukumwe na upepo.


MV Magogoni ilikuwa ikitoka Kigamboni kuelekea upande wa pili (ferry) huku ikiwa na abiria zaidi ya 100 na kusababisha hofu kwa abiria na kusababisha baadhi ya abiria hao kukimbilia vifaa vya kuogelea hata hivyo mainjinia waliokuwa ndani ya kivuko hicho walifanya jitihada za kuwasha injini moja ya kivuko hicho na hatimayekuendelea na safari.

No comments:

Post a Comment