Sunday, January 27, 2013

PICHA TISA ZINAZOONYESHA ATHARI ZA VURUGU MKOANI MTWARA

Ofisi ya Elimu wilaya ya masasi ikiteketea kwa moto kufuatia vurugu za wananchi zilizotokea jana wilayani humo kwa kile kilichodaiwa askari kumpiga mwendesha bodaboda na kusababisha kifo chake.
Baadhi ya magari ya Halmashauri ya wilaya masasi yakiteketea kwa moto
Gari la wagonjwa la wilaya ya masasi nalo likiteketea kwa moto
Jenereta la Halmashauri hiyo poa likiteketea kwa moto
Nyumba ya Waziri wa Tamisemi Mh. Hawa Ghasia, iliyopo maeneo ya stand mtaa wa Sinani mkoani Mtwara jinsi ilivyoteketezwa kwa moto sambamba na kuvunjwa kwa vioo vya madirisha na milango kama inavyoonekana pichani.
Pichani ni jinsi mahakama ya mwanzo iliyopo mtaa wa stand kata ya Chikongola ilipokuwa inaanza kuteketea kwa moto, inasemekana kuwa eneo hilo lililopo mahakamani hapo limeuzwa na kuuziwa mtoto wa Rais Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Ridhiwan Kikwete.
Mabaki ya mahakama ya mwanzo ilivyoteketezwa na wananchi wenye hasira kali wilayani Mtwara.
Moja tu kati ya mabango wakati wa maandamano kabla hawajaamua kuanzisha vurugu
Mkazi wa Magomeni mkoani Mtwara Mohamed Rashid akiwa amejeruhiwa kutokana na vurugu hizo.

 

















HABARI KAMILI
WATU Saba akiwemo askari polisi mmoja wameuawa katika vurugu zilizotokea jana wilayani Masasi mkoani Mtwara, zikiwa zimebeba sura ya kupinga gesi kwenda Dar es Salaam.

Muuguzi wa zamu hospitali ya wilaya ya Masasi, Mkomaindo Fatuma Timbu amethibitisha kupokea maiti za watu saba.

Majeruhi ambao idadi yao haijajulikana wamekimbizwa hospitali ya misheni ya Ndanda kwa matibabu na hali bado ni tete, Vurugu kubwa zilianza majira ya saa 4 asubuhi jana baada ya polisi waliokuwa wakiendesha pikipiki kumgonga mtu na kukataa kutoa ushirikiano, Hata hivyo hoja hiyo ilihamia kwenye suala la gesi na kundi la vijana mara moja walivamia nyumba ya mbunge wa Masasi, Mariam kasembe na kuiwasha moto, pamoja na magari mawili.

Aidha vijana hao walivamia nyumba ya Anna Abdallah na kuiteketeza kwa moto kabla ya kuivania ofisi ya CCM wilaya na kuichoma moto pamoja na magari matatu, Hasira za wananchi hao zilifika kituo kidogo cha polisi kilichopo Mkuti wilayani humo na kukichoma moto ambapo baadae walichoma moto magari matano ya halmashauri ya wilaya.

Pia walichoma moto ofisi ya elimu ya halmshauri ya wilaya Masasi vijijini, kabla ya kuichoma ofisi ya maliasili.

Polisi kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya mkoa wa Mtwara inadaiwa walitumia risasi za moto na kusababisha vifo vya watu Sita huku polisi akidaiwa kuuawa kwa kupigwa na wananchi.

Picha na Happy Severine Mtwara, habari Abdulaziz video Masasi

No comments:

Post a Comment