Friday, January 18, 2013

WASANII WA BONGO MOVIE KUTANGAZWA KIMATAIFA, WAAHIDIWA KUPELEKWA KUPELEKWA NIGERIA KUCHEZA FILAMU

 Mkurugenzi wa Mad Mad Entertainment, Yasmin Razak (katikati) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu kampuni yake kuingia mikataba na wasanii wa filamu wa Tanzania na kuwapeleka Nigeria na Jmahuri  ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kwa ajili ya kutengeza filamu. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Superior Solutions, Issack Kasanga na (kulia) Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifamba. 

Msanii wa filamu, Steve Nyerere (kulia) akifafanua jambo wakati wa mkutano huo.Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Superior Solutions, Issack Kasanga(kushoto) na Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifamba(katikati)

KAMPUNI ya Mad Mad Entertainment iliyopo jijini London nchini Uingereza, 
imeanzisha program maalum ya kupeleka wasanii wa filamu za bongo nje ya nchi kwa lengo la kukuza sanaa hiyo hapa nchini.
 Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Yasmin Razak alisema ameamua kufanya kazi na wasanii  hao ili kuleta mabadiliko na kuwakwamua kiuchumi wasanii wa filamu hapa nchini baada ya kuona sanaa ya Tanzania haikui.

 “Kwa muda mrefu niliokaa London nimeona sanaa ya Tanzania haikui wala haibadiliki, nikafikiria kitu gani nifanye ili  kukuza tasnia hii ndipo nikaamua kuanzisha mpango huu, katika mkataba na kampuni msanii atakayetengeneza filamu na wasanii wa nje atalipwa kiasi cha sh 50 milioni pamoja na malipo mengine yatakayokuwepo kwenye mkataba, ikiwa ni pamoja na asilimia fulani kwa kila kazi itakayouzwa hapa nchini.

“Nimekuwa nikifanya kazi hiyo na wasanii wengi kutoka Nigeria wakiwemo kina Omotola, Two Face na wengineo na pia Ghana, Congo na hata Uingereza, hivyo nimeonelea kuwa itakuwa vema Tanzania nao kuingia katika mchakato huo,”alisema Razak.

Razak ambaye amesema pamoja na kusimamia kazi za muziki za Fally Ipupa lakini sasa wameanza project ya filamu ambapo tayari Fally ameshafanya filamu moja na 2Face Idibia na sasa ameamua kuangalia nyumbani na alitaja vigezo vya msanii atakayechaguliwa ikiwa ni pamoja umaarufu,  kuijua lugha ya kiingereza, uwezo wa kuigiza na kuuvaa uhusika wowote pamoja na mavazi.

Naye rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifwamba aliwataka wasanii hao kujipanga kimataifa zaidi katika kuhakikisha wanaingia kwenye ushindani huo na kuwataka wale watakaochaguliwa kujituma na kutuwakilisha vema kwa kuonyesha nidhamu ya uhakika.

“Hapa kuna kuinua vipaji, soko la kimataifa na mengineyo, hivyo ni vema kufanya kazi kikamilifu kwa wale watakaochaguliwa na si kujisahau, wanatakiwa wasanii watatu na tupo katika hatua za awali za mchujo,” alisema
Mwakifamba.

No comments:

Post a Comment