Friday, January 18, 2013

NASEMA UKWELI SIJUI KIINGEREZA AFUNGUKA CLOUD



Staa wa filamu nchini Issa Mussa(Cloud) pichani, aliwaacha watu midomo wazi pale alipoamua kufunguka mbele ya hadhara ya watu kuwa hajui kiingereza

Tukio hilo lililowashangaza wengi wakiwemo wasanii wenyewe limetokea jana katika ofisi za Finance Solutions wakati wa mkutano wa Mkururugenzi Mtendaji kampuni hiyo(Finance Solutions) Bw. Isaack Kassanga, Mkurugrnzi wa Mad Mad Entertainment Yasmine Razack walipokuwa wakitambulisha mpango wao wa kuwapeleka wasanii nje ya Nchi kufanya Filamu na wasanii wa kimataifa

Wakati wa mkutano huo mkurugenzi wa mad mad Entertainment alisema kuwa kigezo kikubwa kati ya vigezo wanavyotakiwa kuwa navyo wasanii ni kufahamu Lugha ya kiingereza ili iwarahisishie mazungumzo, ndipo msanii huyo alipofunguka kuwa kigezo hicho kisiwe muhimu kwa kuwa wasanii wengi akiwemo yeye hajui kiingereza.

"Nasema ukweli wasanii wengi hatujui kiingereza, nasema ukweli mbele ya waandishi wa habari hata mimi mwenyewe sijui kiingereza kwa hiyo kigezo hicho kisiwe muhimu  kwa sababu wasanii wengi tutakosa nafasi hiyo". Alisema msanii huyo.

No comments:

Post a Comment