Tuesday, March 27, 2012

MAZISHI YA ALIYEKUWA MKUU WA WILAYA YA LIWALE PAUL CHIWILE

Rais Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal, Waziri mkuu Mh.Mizengo Pind, Mkuu wa Mkoa wa pwani Mwantumu Mahiza na Mkuu wa Mkoa wa Lindi wakiwa kwenye mazishi ya aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Liwale Marehemu Paul Chiwile huko Kibaha picha ya ndege
Rais Jakaya Kikwete akitoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Liwale marehemu Paul Chiwile

Rais Jakaya Kikwete akiweka shada la maua kwenye kaburi la aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Liwale Marehemu Paul Chiwile wakati wa mazishi.

Marehemu Paul Chiwile (kulia) enzi za uhai wake akiwa na mkuu wa wilaya ya Kilwa Nurdin Babu katika moja ya mikutano.

Marehemu Paul Chiwile (kulia) wakati wa uhai wake akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Lindi bw. Ludovick mwananzira wilayani kwake Liwale.
Marehemu Paul Chiwile alifariki ghafla siku ya Ijumaa akiwa katika chumba alichofikia Hotel ya Vision iliyopo Lindi mjini na kuzikwa jana huko nyumbani kwake wilayani Kibaha mkoani Pwani.. Mwenyezimungu ailaze Roho ya marehemu mahali pema peponi, Amina.

Habari: na mdau AbdulAziz Ahmed kutoka Lindi.

No comments:

Post a Comment