Tuesday, March 27, 2012

MAMBO YA KALUNDE BAND

Weekend niliwatembelea Kalunde Band pale Trititi Hotel Oysterbay ambapo wanapiga kila Ijumaa nikasema nikuonjeshe na wewe yale niliyoyaona mimi walau kwa picha tu
Hicho kinaitwa Kipaji toka moyoni
Raha ya kuimba uimbe kwa hisia kama hivi

Unaambiwa siyo kuimba tu hata kucheza pia wanaweza
Huyu ni mmoja kati ya wanenguaji wao wawili ila huwa wanasafiri sana kwa ajili ya show zingine za Uarabuni, hivyo wanatafuta wanenguaji wengine wasichana wawili wa Permanent ambao watakuwa wanapamba show zao hata kama hao wengine wakiwa wamesafiri Show zao ziweze kunoga si unajua tena wanenguaji nao wana raha yake stejini.. Hivyo kama una mtu unayemjua mkali kwa unenguaji mpe Tip hiyo alambe ajira wanasema undugu ni kufaana na siyo kufanana, mimi nimeplay party yangu na wewe cheza ya kwako kwa kuwaambia wengine usiwe mchoyo.
Hiki ndo kilimuumiza vidole Nape wakati akijifunza kupiga na anasema katika vitu hawezi kuvisahau ni Gitaa, kaka zangu na nyie vipi hakijawaumiza vidole kweli??? hahahhahha
Kipaji hicho kaka, kupiga kinanda na kuimba si mchezo ingawa wapo wengi wanaoweza lakini wapo pia wanaoshindwa.. Salute kwako
Muimbaji na Meneja wa Bendi Deborah Nyange mwenye chuichui, huyu dada ana sauti kama Chirikuu utasikia mambo yake kwenye Afrobeat Kopi kale... Stay tuned
Shabiki mzuka ukampanda nae akaenda kutoa Support kwa mnenguaji.. Usikose mambo haya ndani ya Afrobeat wee endelea kuangalia tu kila Jumamosi saa moja jioni, Jumapili saa 11 jioni na ukikosa kote huko tega jicho lako Jumatano saa 6 mchana.

No comments:

Post a Comment