Tuesday, March 27, 2012

ANNA PETER WA EAST AFRICA RADIO ATEMBELEA KITUO CHA WATOTO YATIMA CHA GUARDIAN ANGEL


Jumamosi iliyopita mtangazaji wa kipindi cha Power Jams ya East Africa Radio, Anna Peter alitembelea kituo cha kulelea watoto yatima cha Guardian Angel kwa ajili ya kufanya mahojiano na Watoto wa kituo hicho pamoja na Uongozi ili waweze kupata msaada wanaouhitaji (Pichani ni Anna Peter akifanya mahojiano na watoto hao)
Anna Peter katika picha ya pamoja na mkurugenzi wa kituo Miriam Msangi(Kulia) pamoja na watoto wanaolelewa katika kituo hicho
Anna, mlezi wa watoto hao pamoja na watoto wenyewe... Watoto hawa bado wanahitaji msaada wa vitu mbalimbali vikiwemo magodoro, vitanda na chakula hivyo kama unahitaji kutoa msaada waweza kuwasiliana na wahusika kwa namba hizi 0757 855858 na 0655 855858.

No comments:

Post a Comment