Monday, November 28, 2011

SIKU YA TELEVISHENI DUNIANI

Novemba 21 kila mwaka ni siku ya Televisheni Duniani hivyo sisi EATV tuliandaa kipindi maalum kwa ajili ya kuadhimisha siku hiyo ambapo tulitoa nafasi kwa watazamaji wetu kushiriki pamoja nasi kwa kutoa maoni yao kuhusiana na siku hiyo na wangependa nini kifanyike katika kuboresha Televisheni duniani!

Hosts wa show hiyo maalum tulikuwa mimi (Kijah) kushoto na Deo kulia

Tulikuwa na wageni pia studio ambao tulishiriki nao kwenye kipindi ambapo pamoja na mdahalo ambao tulikuwa tukiujadili siku hiyo unaosema ni yupi Presenter bora kati ya mwanaume na mwanamke, pia tulirusha makala kutoka kwa baadhi ya wadau wetu wa Televisheni ambao ni TCRA, Kampuni ya simu za mkononi TIGO, MCT, Chuo cha watayarishaji wa vipindi IAMCO na Makala kutoka BBC ambazo zilieleza mambo tofauti tofauti kuhusiana na Televisheni.

Mmoja kati ya mafundi mitambo wa EATV Allan Lyimo akihakikisha mambo yanakwenda sawa

Timu nzima ya watayarishaji wa vipindi nao wakihakikisha kila kitu kinakwenda sawa

Baadhi ya wageni wetu wa siku hiyo, kutoka kushoto ni Joyce Kiria, Leyla Ledd ambae alimuigiza Salama J anavyotangaza na alipatia saaana, anayefuata ni Lucy kutoka ubalozi wa Uholanzi, Deo na Kijah

Baada ya kipindi kumalizika Team nzima tukapiga picha za ukumbusho maana show ilikuwa tight sanaaaaa

Mauzo yakiendelea



Nikianza kutaja majina hapa tutakesha jamani mniwie radhi
Nikiwa na mmoja kati ya wageni wetu Mr. Reinfared Masako mtangazaji mkongwe wa TV Tanzania ana miaka 30 sasa katika hii Tasnia, nikajisogeza na mimi si wanasema fuata nyuki ule asali labda na mimi nitafika alipo.. inawezekana bhana ila jitihada za makusudi zinahitajika
Mamaa wa wanawake Live nae akasema mmh na mimi nijisogeze japo kwa picha tuuu
Joyce na Deo wakafunga kazi na hadithi ikaishia hapooo

No comments:

Post a Comment