Tuesday, November 15, 2011

TWANGA PEPETA KUSHEHEREKEA MIAKA 50 YA UHURU LONDON


Kundi la muziki wa Dansi nchini, African Stars "Twanga pepeta" wanatarajia kupiga show kali jijini London Uingereza katika kusherehekea miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania.
Akizungumza na Blog hii kiongozi wa kundi hilo Luiza Mbutu, amesema baada ya watanzania kuupokea vizuri uzinduzi wa Album yao ya kumi na moja waliyoiita "DUNIA DARAJA" sasa wameamua kupeleka mashambulizi katika jiji la London ili kujumuika na watanzania wanaoishi huko katika kusherehekea miaka 50 ya nchi yao ya Tanzania.

Show hiyo kali itapigwa siku ya Jumamosi ya Novemba 26 mwaka huu ambapo album yao mpya na za zamani pia zitauzwa kwa wapenzi watakaozihitaji.

No comments:

Post a Comment