Wednesday, August 21, 2013

Mjue binadamu mwenye kilo 610



Mfalme wa Saudi Arabia, ameingilia kati mpango wa kumsaidia Raia wa nchi hiyo, Khalid bin Mohsen Shaari ambaye ndiye binadamu mnene na mzito zaidi duniani akiwa na uzito wa kilogram 610, katika mchakato wa kumtibu na kumrudisha katika hali nzuri zaidi.

Kutokana na unene, ukubwa na uzito wake, Khalid hawezi kutembea wala kusogea mwenyewe bila msaada wa kifaa maalum cha kumbeba akiwa katika kitanda chake, na cha ajabu zaidi, Ni mshkaji mdogo tu ambaye umri wake ni kati ya miaka 18 na 20.

 Kwa mujibu wa rekodi za Guiness, Manuel Uribe kutoka Mexico ndiye aliyekuwa akishikilia rekodi ya mtu mzito na mnene zaidi duniani ambapo alikuwa na uzito wa kilo560, Na baada ya kuonekana na kuingizwa katika matibabu, kwa sasa amepungua na kufikia uzito wa kilo 444.

Mfalme Abdullah tayari ametoa amri kuwa Khalid kuhamishwa huko Riyadh kwaajili ya mchakato wa matibabu yake.

No comments:

Post a Comment