Wednesday, August 14, 2013

Chanzo cha mashabiki kutaka kumponda mawe Diamond huko Kenya hi hiki!

Baada ya mashabiki kurusha makopo stejini kisa Diamond kuchelewa kupanda hizi ndio sababu zinazosemekana za kushelewa kwake kupanda

Umati wa watu waliohudhuria show ya Platnum wakirusha makopo stejini baada ya Diamond kuchelewa kupanda hizi ndio sababu zilitajwa kupelekea kuchelewa kwake.

mtandao wa kenya Ghafla umeripoti kuwa Diamond alichelewa kwasababu alikua akijifanya "Diva" pale ambapo kwa maksudi alijichelewesha Tanzania na hivyo kuchelewa ndege kuelekea Kenya.

Baada ya kuchelewa ndege Diamond alidai aletewe ndege binafsi (Private Jet) na National Media Group (NMG) ambapo iliwabidi wafanye hivyo.

Mda mfupi baada ya Diamond kutua Mombasa aligoma ku-check in katika hoteli aliyoandaliwa (Mombasa Beach Hotel)  ambapo ndipo show ilipokuwa ikifanyika na kusisitiza kuchukuliwa presidential  suite White Sands Hotel ambayo iliwagharim mkwanja mrefu NMG.

Baada ya mahitaji yake kukamilishwa ndio Diamond alikubali kupanda stage, na kukitifua mbaya stejini  kwa show ya ukweli na perfomance ya hatari na kuwaachia watu wakiwa na historia isiyofutika leo wala kesho, show ambayo inayoweza kuelezeka kama ni ya ki legendary, Mashabiki walitulia na kuimba nyimbo zake mwanzo mwisho..

No comments:

Post a Comment