Friday, August 23, 2013

Hatimaye GK kurudi kwenye gemu rasmi


Hatimaye baada ya kimya cha muda mrefu Mwanzilishi wa kundi la East Coast Team (ECT) “Crazy Gk” aliyetamba na nyimbo kama sauti ya Manka, miko kumi ya rap, sister sister na simba wa afrika anamipango ya kurudi kwenye game la bongo flava.

Msanii huyo aliyepotea kwa muda mwingi akiwa masomoni sasa anataka kurudi tena kwenye game na atazindua wimbo wake mpya wiki ijayo kupitia radio station tofauti tofauti hapa Tz.

Tusubiri tuone ukimya wake uko vipi, Je ataweza kubamba na kukubalika kama ilivyokuwa hapo mwanzo au watoto wadogo wa sasa watampiga bao...karibu kakka mkubwa!!!

No comments:

Post a Comment