Thursday, December 22, 2011

SALUTE KWA MAJESHI YA ULINZI NA USALAMA TANZANIA KWA KAZI KUBWA WALIYOIFANYA

Wakizunguka huku na kule katika kuangalia usalama
Hawa nao wakiwa wameshuka kwenye magari yao

Kikosi cha kutuliza Ghasia na Jeshi la wananchi wakihakikisha mambo yanaenda sawa(Walifanya kazi kubwa sana hawa jamaa)
Askari wa Jeshi la wananchi TZ (JWTZ) wakiendelea na shughuli ya uokoaji
Askari akiongoza watu kupita katika enneo hilo

Picha hizo zote zinaonyesha namna vikosi vya ulinzi na usalama vikisaidia zoezi la uokoaji wa watu waliopatwa walioathirika na mafuriko katika eneo la Jangwani jijini Dar Es Salaam, ambapo pia Askari hao walifunga utumiaji wa barabara hiyo kwa vyombo vya moto kwa muda mrefu mpaka pale maji yalipokauka, halikadhalika watembea kwa miguu pia walizuiwa kutumia barabara hiyo kwa muda kwa ajili ya usalama wao.

Kwa kweli tunapaswa kuyashukuru sana majeshi yetu kwa namna yalivyoonyesha uzalendo kwa kuacha shughuli zingine zote na kuingilia kati suala hili la maafa ya mafuriko.. SALUTE KWAO.

Nilikuwepo eneo la tukio lakini kwa kazi maalum, hivyo nikashindwa kupiga picha lakini namshukuru Ankal michuzi kwa kuniwezesha mimi kupata Picha kupitia michuzi.blogspot

No comments:

Post a Comment