Tuesday, December 20, 2011

KANUMBA ADAIWA KUPOTEA KWENYE MISITU YA YANGADOU REINFOREST HUKO CONGO

Kuna habari zimeenea kwenye mitandao kuwa Movie star wa Bongo Steven Kanumba (Pichani)amepotea huko katika misitu inayofahamika kama Yangadou Reinforest Jamhuri ya watu wa Kongo, alipokuwa akishoot Movie mpya inayoitwa Mother Land.
Habari hiyo imeendelea kusema kuwa Kanumba alipotea kwa saa 24 tangu siku ya Dec 19, 2011 baada ya kugombana na Director wa Movie hiyo na yeye (Kanumba) kuamua kuondoka katika eneo hilo ambalo walikuwa wameweka kambi kwa ajili ya Kushoot Movie hiyo na mpaka masaa 24 baadae alikuwa hajaonekana hali iliyopelekea wenzake kuanza kumtafuta kwa kutumia Helikopta bila ya mafanikio lakini pia inasemekana kuwa katika misitu hiyo kuna kundi la waasi ambao wanaishi na wamekuwa wakipoteza maisha ya watu mara kwa mara.

Baada ya kuisoma habari hii ilibidi nimtafute Kanumba kwa njia ya simu ili kufahamu ukweli wa jambo hili na mwenyewe akathibitisha kuwa yeye yupo hapa hapa Bongo na taarifa hizo siyo za ukweli.. Nimeshusha pumzi sasa baada ya kuongea nae maana mmh niliogopaaa.

No comments:

Post a Comment