Thursday, December 22, 2011

MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM AMEWAASA WANANCHI KUTOA MISAADA KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO

Baadhi ya waathirika wa mafuriko wakisubiri kuokolewa

Nyuma ambayo imeathirika kutokana na mafuriko hayo

Hapa ni Airport DSM hali ilivyokuwa jana

Hali bado ni tete na baadhi ya watu wakijaribu kuokoa maisha yao na ya watoto
Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Said Mecky Sadick akizungumza na vyombo vya habari.
Hali bado ni tete katika jiji la Dar Es Salaam kama ambavyo vyombo mbalimbali vya habari vimeripoti kuhusiana na janga la mafuriko lililoathiri Familia nyingi sana kwa kupoteza makazi yao na maisha ya ndugu zao kutokana na mvua iliyonyesha kwa siku ya tatu leo mfululizo.

Kama ambavyo tunafahamu linapotokea janga kama hili panahitajika misaada mingi sana kama vile maji, chakula, mavazi, n.k. hivyo Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Bw. Said Mecky Sadick amewaomba wale wote wenye lengo la kutoa msaada wapeleke misaada hiyo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa iliyopo Ilala Boma jijini Dar Es Salaam.

Bw. Sadick amezungumza hayo wakati wa mahojiano maalum aliyoyafanya na East Africa Radio katika walipotaka kufahamu mambo mbalimbali yanayoendelea kutokana na maafa hayo yaliyoikumba Taifa.

Picha kwa hisani ya Eatv no.1 Youth Channel

No comments:

Post a Comment