Monday, September 2, 2013

The Chocolate waibuka washindi wa Dance 100, 2013



Shindano la kucheza linalo fahamika kama DANCE 100% jijini dar-es salaam limekamilisha mpambano wake katika uwanja wa DONBOSCO OYSTEBEY siku ya tar:31-08-2013.

Mashindano hayo yalianzia(USAILI) katika uwanja wa DONBOSCO UPANGA,TTC CHANG”OMBE na kumaliziwa DONBOSCO OYSTEBEY jana.

Ylikuwa makundi mengi sana ila kati ya hayo yaliofanikiwa kuingia hadi fainali ni makundi matano 5 tu nayo ni :D DI,WT(watoto wa Tanzania),WAKALI SISI,THE CHACOLETE na THE WINNERS pia kulikuwa na mizunguko miwili ambao wa kwanza walicheza wimbo walio chagua (wahusika wa kuu wa kundi husika ) na mzunguko wa pili ilikuwa wimbo uliochaguliwa kwa bahati na sibu na wahusika wa kuu wa kundi husika kwa kuokota CD ambozo waandaaji  waliziandaa

Yalio kuwa yanahitajika ni makundi matatu tu,THE WINERS wakatoka na kubaki yale yalio kidhi vigezo kwa maksi za majaji:WAKALI SISI walishika namba 3.walipata zawadi ya shilingi 500,000 za kitanzania,DDI wakashika namba 2 walipata zawadi ya shilingi 1,500,000 za kitanzania na THE CHOCOLETE ndio walio ibuka namba 1, na kuchukua kitita cha zawadi ya shilingi 5,000,000 za kitanzania toka Vodacom Tanzania.

No comments:

Post a Comment