Thursday, September 5, 2013

Hemedy PHD atangaza kuacha kuvaa hereni

Kupitia ukurasa wake wa mtandao mmoja wa kijamii mwigizaji Hemedy Suleiman maarufu kama Hemedy au Fernando (a.k.a yake mpya) amesema kuwa hatavaa tena hereni kwenye kuigiza kwani ameshakuwa mtu mzima sasa.

Hemedy ambaye hivi majuzi alisherehekea kutimiza miaka 27 ya kuzaliwaameandika kuwa kama mtu mzima, hata vaa tena hereni katika movie zake.

Hatujaweza kujua kama ataacha kabisa kuvaa hereni au ni kwenye uigizaji tu.


Ila hapo nyuma mwezi uliopita wakati msanii huyo akichat EATV katika kipindi cha KIKAANGONI LIVE aliweza kusema kuwa amejifunza mengi na moja ya jambo alilojifunza ni kuwa mashabiki zake hawapendi yeye avae hereni wakati anaigiza, kwahiyo hiyo inaweza ikawa sababu ya Hemedy kuamua kuacha kuvaa hereni

No comments:

Post a Comment