Tuesday, March 19, 2013

ZAIDI YA ASILIMIA 75 YA WAKAZI WA DSM HAWAANGALII TV TANGU ULIPOANZA MFUMO WA DIGITAL


Tangu Tanzania ilipohamia katika mfumo wa Digital mapema mwaka huu ni zaidi ya asilimia 75(75%) ya wakazi wa Dar Es Salaam hawaangalii Televisheni kutokana na kukosa uwezo wa kugharamia ving'amuzi.

Utafiti uliofanywa na wamiliki wa vyombo vya habari Nchini(MOAT) umeonyesha kuwa kwa Mkoa wa Dar es salaam pekee, zaidi ya asilimia 75 ya  wakazi wa jiji hilo hawaangalii channel za TV majumbani kwao tamhu ulipozimwa mtambo wa analog na kuanza kutumika mtambo wa digital na kusababisha umoja huo kuitaka serikali kuangalia upya uwezekano wa kurudisha matangazo ya analog kwanza mpaka Watanzania watakapozoea Digital.

Akizungumza jijini DSM mwenyekiti wa MOAT Dr. Reginald Mengi alisema, “Watanzania wapewe muda kujiandaa ili kutoka analog kwenda digital ifanyike vizuri na kwa mafanikio makubwa, pendekezo letu lilikua ni kwamba analog na digital ziende sambamba mpaka tufike mahali tuone kwamba watu wengi kama sio wote wana vyombo vya kuwawezesha kwenda digital, hilo lifanyike kabla ya tarehe 17 june 2015 ambayo ndio siku ya mwisho ya kutumia analog”

No comments:

Post a Comment