Tuesday, March 26, 2013

WEMA ASITISHA KUZUNGUMZIA KUHUSU KUMLIPIA FAINI KAJALA


Wema akiwa na Kajala mara baada ya kuachiwa huru kwa Kajala
Baada ya mlimbwende Wema Sepetu kumnusuru msanii mwenzake Kajala kifungo cha miaka saba kwa kumlipia Faini ya Tshs Milioni 13 na vyombo mbalimbali vya habari hapa Nchini kuiripoti taarifa hiyo, Mwanadada huyo ambae ni Staa wa Filamu hapa Bongo amesema ameshaufunga mjadala huo na hayuko tayari kuendelea kulizungumzia suala hilo.

Akizungumza na Blog hii msanii huyo amesema aliamua kumsaidia Kajala kwa moyo wake na kama rafiki yake lakini hakuwa na nia ya kufanya Publicity kama inavyofanywa na vyombo vya habari na kuongeza kuwa kwa ambao tayari wameshafanya hivyo sasa imetosha na binafsi hayuko tayari kuendelea kulizungumzia suala hilo kwani kwa kufanya hivyo atakuwa kama anamsimanga rafiki yake huyo au anajisifu kwa kile alichokifanya kitu ambacho anaona hakitaleta picha nzuri na kitazusha mjadala mwingine kwa jamii.
Kajala alishikiliwa na Polisi na kuwekwa mahabusu mwaka jana kwa kudaiwa kuwa yeye na mumewe Faraja Chambo walikula njama ya kuhamisha umiliki wa nyumba iliyopo Kunduchi Salasala jijini Dar es Salaam,  kinyume na kifungu cha 34 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007,
Pia ilidaiwa kuwa Aprili 14, 2010, walihamisha umiliki wa nyumba kinyume na Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa na katika shitaka la tatu kuwa Kajala na mumewe walidaiwa kuwa  Aprili 14, 2010, wakijua kuwa ni kinyume na sheria, walifanya kosa la kutakatisha fedha haramu.

No comments:

Post a Comment