Friday, March 22, 2013

MASHUJAA MUSICA WAKANUSHA UVUMI WA CHARLES BABA KUTIMKIA TWANGA


Uongozi wa Mashujaa Band, umesema uvumi ulioenea mtaani kuwa mwanamuziki Charles Baba (pichani) ambae pia ni Rais wa Bendi hiyo ameihama Bendi hiyo na kurudi Twanga alikokuwa akifanya kazi kabla ya kujiunga na Mashujaa si wa kweli ni wa uzushi.

Mkurugenzi wa Bendi hiyo Sakina Mbange maarufu kama Mamaa Sakina alisema kuwa maneno hayo yaliyoenea mitaani ni ya kizushi na kufunguka kuwa ni kweli mwanamuziki huyo pamoja na mwanamuziki mwingine mpiga Tumba maarufu wa bendi hiyo(Mashujaa)  MCD waliwahi kupanda katika jukwaa la Twanga pepeta lakini haimaanishi kuwa wanamuziki hao wamejiunga na Bendi hiyo.

Akizungumza na Blog hii mwanamuziki Charles Baba nae alikanusha vikali uvumi huo na kuwataka mashabiki wake waondoe shaka na kuwahakikishia kuwa bado yeye ni mwanamuziki wa Mashujaa na ana mkataba wa kuitumikia Bendi hiyo na hana mpango wa kuhamia Bendi yoyote nyingine.

Hata hivyo wiki chache zilizopita Charles Baba alizungumzia pia uvumi huo wa yeye kuhamia Twanga Pepeta na kukiri kuwa ni kweli alionekana kwenye jukwaa la Twanga Pepeta kwa ajili ya kujikumbusha na kuonyesha mashabiki kuwa hana Bifu na mkurugenzi wa Bendi hiyo Asha Baraka wala wanamuziki wa Bendi hiyo kama ambavyo wadau wa muziki wanafikiria.

No comments:

Post a Comment