Monday, June 24, 2013

OMMY DIMPOZ ALIVYOPIGWA MAKOPO DODOMA AIITA 'MAKOPO STYLE'

Msanii Ommy Dimpoz ambaye alipondwa na makopo ya vinywaji mjini Dodoma juzi katika show ya KILI MUSIC TOUR 2013, tayari ameipa jina staili hiyo kupitia ukurasa wake wa Twitter

"ha ha ha hiyo ni Makopo style ukirusha Nakwepa nikilidaka nakupa nalo la uso", hayo ni maneno aliyotweet Ommy Dimpoz leo asubuhi wakati akichat na baadhi ya watu.

Pia akiendelea kutweet amesema kuwa sasa amejipanga kamili kwa mashabiki wote watakaorusha hizo vitu akiwa stejini.

"hahahahaha kuna moja nililirudisha na teke nikasikia shabiki kapiga yowee YALAAAA nikajua litakuwa la kichwa hilo".

Dah, hii kali sasa, patamu hapo. Na wadau wengine wameipa staili hiyo jina la 'Rusha nikwepe Ooo me n you'
.

No comments:

Post a Comment