Tuesday, August 30, 2011

AUAWA KIKATILI AKIDAIWA KUIBA KUKU

Kijana aliyefahamika kwa jina la Xavery Naseeb maarufu kama Mkemia akiwa amechomwa moto katika eneo la Viwanja vya shule ya msingi mwenge jijini Mbeya kwa tuhuma za kuiba kuku

Marehemu Xavery akiwa amelala pembeni mwa kuku aliodaiwa kuiba

Marehemu Xavery

Askari wa Jeshi la polisi wakiwa katika eneo la tukio kuuchukua mwili wa marehemu kwa ajili ya kuupeleka Hospitali ya Rufaa Mbeya.
 Kutoka kwa afrokija: Ni kosa kujichukulia sheria mkononi hata kama kuna ushahidi wa Tukio kama hilo, ni vema kutumia vyombo vya Dola kwa kuwa vyombo hivyo vipo kwa kazi hiyo. Hebu fikiria kama huyo aliyefanyiwa hicho kitendo hiki angekuwa ni ndugu yako ungejisikia vipi?? hupaswi kumtendea mwenzako jambo ambalo usingependa kutendewa.. Pia iwe fundisho kwa vijana wenye tabia hizo za wizi kwani vina madhara makubwa, na tujifunze kwa haya yaliyompata ndugu yetu Xavery.. 

Blog hii inatoa pole kwa ndugu, jamaa na Marafiki wa marehemu Xavery na mwenyezimungu aiweke mahali pema roho ya Marehemu, Ameen.

Picha: kwa Hisani ya Mbeya yetu blogspot

ANSWAAR SUNNA WALIVYOSWALI EID YAO LEO KATIKA VIWANJA VYA JANGWANI

Sheikh Juma Polli Amir wa Answaar Sunna Tanzania akiongoza swala ya Eid El-fitri leo katika viwanja vya Jangwani jijini Dar Es Salaam
Waumini wa Dini ya Kiislamu wa Dhehebu la Answaar Sunna wakisikiliza mawaidha baada ya swala ya Eid El-Fitri leo katika Viwanja vya Jangwani-DSM

KALUNDE BAND WANAKUJA STYLE YA MDUARA

Bendi ya Muziki wa Dansi nchini, "Kalunde Band" inatarajia kutambulisha wimbo wake mpya wa mduara katika maonyesho yake yote ya Sikukuu ya Eid El-fitri, ambao umetungwa na na mpiga kinanda wa bendi hiyo Mwakichui Saleh.

Kiongozi wa Bendi hiyo Bob Rudala (Pichani) amesema wimbo huo umepewa jina la "Imebaki Story" ambao ni miongoni mwa nyimbo mpya zilizokamilika hivi karibuni kwa ajili ya Album yao ya pili.
Ameongeza kuwa wimbo huo utatambulishwa siku ya Eid Mosi katika Onyesho lao la ukumbi wa Trinity uliopo Oysterbay jijini Dar Es Salaam na kisha kutambulishwa Eid pili katika ukumbi wa New kunduchi Beach Hotel.

Monday, August 29, 2011

MASHAUZI CLASSIC YASHAURIWA KUBADILI JINA

Kundi jipya la Muziki waTaarab nchini lenye maskani yake kinondoni jijini Dar Es Salaam (Mashauzi Classic) linaloongozwa na Isha Ramadhani a.k.a Isha Mashauzi limeshauriwa kubadili jina hilo na kutafuta jina lingine litakalotafsirika kirahisi ili kusaidia kundi hilo kupata umaarufu mapema.

Ushauri huo umetolewa na Waziri mkuu Mstaafu Bw. John Samwel Malecela (pichani) kwa madai kuwa, kwa mtazamo wake anadhani kuwa jina hilo haliwezi kuteka haraka soko la muziki kibiashara na kushauri kuwa jina hilo libadilishwe.
Akizungumza jijini Dar Es Salaam mlezi wa kundi hilo ambalo linatarajiwa kuzinduliwa rasmi siku ya Eid Mosi katika ukumbi wa Travel Tine jijini Dar Es Salaam Bw. Juma Mbizo (pichani) amesema, baada ya kutoa ushauri huo Malecela amependekeza kundi hilo litumie majina ya Mwanasesele au Mzalendo na kuongeza kuwa uzuri wa kundi ni pamoja na jina na hata kibiashara suala la jina lina umuhimu mkubwa ambapo alitolea mfano Bendi ya African Stars "Twanga pepeta" kuwa limefanikiwa kuteka soko la burudani kwa kuwa jina lake linauzika.
Hata hivyo Juma Mbizo alisema kuwa si lazima ushauri huo ufuatwe kwa kuwa inafahanika kuwa jina hilo la Mashauzi limetokana na jina la kisanii la Mmiliki na Mkurugenzi wa kundi hilo ambalo hata hivyo Malecela hana uhakika kama litateka soko la Mashabiki kwa kasi.




Sunday, August 28, 2011

NMB YATOA MSAADA WA MAGODORO 40 KATIKA HOSPITALI YA WILAYA KILWA MKOANI LINDI

Kaimu Mkurugenzi wa H/Wilaya Kilwa Bw Ndumbalo akikabidhi moja ya godoro kwa Mganga Mkuu wa Hospitali ya wilaya Kilwa
Meneja wa NMB kanda ya kusini Bw Thomas Kilongo akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kilwa moja kati ya magodoro yaliyotolewa na Benki hiyo
Mmoja kati ya wauguzi wa wagonjwa waliolazwa katika Hospitali hiyo akifua mashuka yanayotumika Hospitalini hapo


Habari kwa Hisani ya Mdau Abdulaziz kutoka Lindi



MERCY JOHNSON SASA NI PRINCESS

Katika ndoa ya kimila Prince & princess Okojie wakiwa na furaha

Mambo yakanoga zaidi kwa ndoa ya kanisani

Kuolewa raha jamani

Mambo ya makeup hayo

Mercy ndani ya Shella

Hayawi hayawi sasa yamekuwa, baada ya vikwazo vya hapa na pale viliwavyotia mashaka baadhi ya watu wakiwemo mashabiki wa Mercy wakihofia kutofungwa kwa ndoa ya Mercy Johnson na Prince Odianosen Okojie hatimaye ndoa hiyo tayari imefungwa.

Kikwazo kiliibuka baada ya mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Lovely Okojie kujitokeza na kudai kuwa yeye ni mke halali wa Prince huyo ambapo siku chache baadae ikathibitishwa kuwa ndoa ya Mercy na Prince Okojie itafungwa kama kawaida kwa kuwa mwanamke huyo mwenye watoto wawili tayari alikwishaachika miaka kadhaa iliyopita.

 Ndoa ya Mercy Johnson na Prince Okojie imefungwa juzi jumamosi katika kanisa la Christ Embassy Church lililopo jijini Lagos nchini Nigeria baada ya kufungwa kwa ndoa ya kimila siku ya Ijumaa hukohuko jijini Lagos.

BREAKING NEWS: MAFURIKO YAUA WATU ISHIRINI NCHINI NIGERIA


Hali ni tete
Magari yakiwa yamezidiwa na maji
 
 Waendesha pikipiki nao wakiokoa maisha yao



 Akina mama na watoto nao wakijaribu kuokoa maisha yao
Mvua nyingi iliyosababisha mabwawa kujaa isivyo kawaida na kusababisha baadhi ya nyumba kuzama imeua watu ishirini na kuwaacha maelfu wengine wakiwa hawana makazi huko kusini magharibi mwa Nigeria katika jiji la Ibadan, Mvua hiyo kubwa ilianza kunyesha siku ya ijumaa iliyopita.
Mafuriko hayo yayolitokana na takataka kuziba mifereji ya maji baada ya mabwawa kufurika yamesababisha kuvunjika kwa madaraja, magari kuzama na watu kutembea umbali mrefu kutoka katika maeneo yao na kwenda kutafuta hifadhi katika maeneo mengine.

Friday, August 26, 2011

Thursday, August 25, 2011

HII NDIYO LINDI YETU TWAJIDAIA WENYEWE

Hapa ndo City Center jengo linaloonekana ni CRDB Bank na kwa upande wa pili ni Soko kuu la Lindi wenyewe twaita Soko kubwa

Huu mtaa upo maeneo ya Posta ukiinyoosha huko mbele unakuta Stand kuu ya Mabasi

Hapa ni maeneo ya Police Linena hii inayoonekana kwa mbele ni karakana yao

Hapa ni Ofisi ya Posta sehemu ya kuingilia

Huu mtaa upo maeneo ya sokoni na hii ni barabara ya kuelekea Hospitali ya Mkoa yaitwa Sokoine na Kwa mbali namuona Rama Kindamba ni Mgonjwa wa akili maarufu kule Lindi (Huu mtaa ndio kwao swaiba wangu Sada Kadhi)

Hapa mitaa ya Uhindini yaani maeneo haya wanaishi wahindi sana waswahili ni wachache tu wa kuhesabu na ukinyoosha kule mbele unaelekea Stand kuu ya Mabasi pia

Jengo hili maarufu sana na hadi haya maeneo tulikuwa tunayaita kwa TAHFIF lakini pia ukivuka tu barabara upande wake wa pili ni Soko kuu(Nakumbuka hapa palikuwa maarufu sana kwa kinywaji Togwa maana wauzaji walikuwa wanajipanga hapo mida ya mchana hadi jioni, I mic Togwa jamaniiii)
Hapa wapi vileeeeeeee mbona sikumbukii
Hii ni ofisi ya TTCL na iko maeneo ya Posta
Ahsante kaka OTHMAN MICHUZI wa Blog ya mtaa kwa mtaa kwa kuikumbuka Lindi yetu, yaani nimefurahi sana kuona Mandhari ya Lindi yetu kwenye Blog yako ila mbona hujafika maeneo ya kwetu Wailes jamaniii?? Ila nimekumbuka mbali saaaanaaaa naamini wana Lindi wenzangu kama Sada Kadhi, Joseph Mahundu, Mwl Mussa Utaly, Shaibu Bao na wengineo mtakuwa mmefurahia pia.


                                              I LUV LINDIIIIIIIIIIII!!!!!



WAFAHAMU WAIGIZAJI WA KIKE 15 AMBAO NI GHALI HUKO NIGERIA

Msanii kiwango kabisa ni GENEVIEVE NNAJI (Pichani), ambaye hulipwa Naira 2Millions kwa Script

Anaeshika namba mbili ni IDI EDO hapo juu ambae analipwa Naira 1.8 Million kwa Script

PATIENCE OZOKWOR ni namba 3 anachukua N 1.6 Million kwa Script

OMOTOLA JALADE ndo anashika namba 4 ambae ujinyakulia N 1.5 M kwa Script na kuendelea.

Huyu ni KATE HANSHAW kwa upande wake hulipwa N 1Million kwa Script

STELLA  DAMASUS anachukua kiasi chochote ambacho kwa upande wake anaona kinakidhi mahitaji  lakini ni zaidi ya N 1Million

JOKE SILVA ambae hulipwa N 1  Million kwa Script

NGOZI EZEONU nae analipwa N 1Million Per Script

RITHA DOMINIC nae pia N1 Million kwa Script


CHIOMA CHUKWUKA kwa upande wake bila N 700,000 kwa Script hawezi kucheza Movie yako

OGE OKOYE yeye anachukua N 600,00

FUNKE AKINDELE bila N600-700,000 bado hujamuuzisha sura kwenye Movie yako

MERCY JOHNSON ambae ana make  Headlines kwa sasa kutokana na ndoa yake inayotarajiwa kufungwa hivi karibuni, kwa upande wake analipwa N 600,000 Million

FATHIA BALOGUN hapo juu hulipwa N500,000M kwa Script

UNCHE JOMBO ndo anatufungia ambae analipwa N450,000 M per Script
Kama nilivyoeleza hapo juu, hawa ni waigizaji 15 wa huko Nigeria ambao ni ghali zaidi ya wengine na tumejionea namna ambavyo wanalipwa katika kazi yao hiyo ya uigizaji, na kwa kweli tunaona wenzetu jinsi walivyo na maisha mazuri ya kifahari na ya kujivunia kwa kazi yao kwa kifupi tu tunaona kama si kusikia wakibadilisha magari ya kifahari kila kukicha, mavazi ya thamani yanayowafanya wawe na muonekano maridadi mara zote na mengineyo. Lakini nafikiri haya yanatokana na umakini wao katika kazi wanazozifanya, sasa changamoto ni hapa kwetu bongo sina hakika sana na malipo yao but kwa kweli kwa mavazi tu tunaona pia hapa kwetu wanajitahidi kwa kupiga pamba lakini mengine hali halisi tunaiona, sitaki kusema meeeengi lakini hii tuichukulie kama Changamoto ya kuboresha kazi zetu na kuwa makini.      

Sunday, August 21, 2011

HATIMAYE MASHAUZI CLASSIC IMETAMBULISHWA RASMI KWA WANAHABARI NA WADAU WAKE

Mlezi wa Mashauzi Classic JUMA MBIZO akizungumza na wanahabari

Mkurugenzi ISHA RAMADHANI akiitambulisha rasmi timu ya Mashauzi Classic

Wanamuziki wanaounda Mashauzi Classic

Wanahabari busy na kazi yao
Bendi mpya ya Muziki wa Taarab nchini, "Mashauzi Classic" imetambulishwa rasmi kwa wanahabari na wadau wa muziki huo kwa ujumla jumamosi iliyopita.

Mkurugenzi mtendaji wa kundi hilo Bi ISHA RAMADHANI a.k.a ISHA MASHAUZI amesema wameamua kutambulisha kundi hilo kwa wadau baada ya kuhakikisha kuwa wamejipanga vema na wako tayari kutoa burudani ya uhakika kwa mashabiki wake.
"Kundi hili limeanza muda mrefu kidogo na tulikuwa tukitoa burudani kimya kimya kwa mashabiki wetu lakini sasa tumaamua kujitambulisha baada ya kuhakikisha kuwa tumejipanga vizuri na tuko tayari kutoa burudani ya uhakika kwa mashabiki wetu na tutazindua rasmi siku ya Eid mosi katika ukumbi wa "Travel Tine Hotel" alisema Isha.

Isha aliongeza kuwa baada ya kutoa burudani ya nguzu siku ya Eid Mosi, Eid pili watakuwa Kigamboni, Eid tatu Kibaha, Eid nne watakuwa Kawe na Eid tano wataporomosha burudani kwa mashabiki wa Ukonga.

Aidha kundi hilo tayari limekamilisha Album mbili, Album ya kwanza ikiwa na vibao vinne ambavyo ni" nani kama mama" ambacho kimebeba jina la Album, baraka za baba, Mamaa Mashauzi mtoto kutoka Musoma na Umdhaniaye ndiye kumbe siyo na katika Album ya Pili kuna nyimbo tano ambazo ni Hakuna kati yenu wa kunirusha roho, La mungu halina muamuzi, Niacheni nimpende, Sitosahau kwa yaliyonikuta na anayejishuku hajiamini.

Kundi hilo linaundwa na wanamuziki 22 akiwemo Isha mashauzi ambaye ni mkurugenzi, Bi Rukia Juma (Mama mzazi wa Isha) Kaimu Mkurugenzi, Thabit Abdul Mkurugenzi wa mipango Juma Mbizo Mshauri na Mlezi wa kundi na Wanamuziki wengine wakiwemo wapiga vyombo na waimbaji.